Posts

Mitindo Yetu Ya Ulaji.

Image
MITINDO YA ULAJI Viumbe hai vyote akiwemo na mwanadamu huitaji chakula ili kuishi. Mwanadamu ana mahitaji makuu matatu na chakula ni hitaji muhimu zaidi ya mengine ambayo ni mavazi na malazi. Kwa umuhimu wa chakula, mwanadamu huitaji kula kila siku. Na inapotokea hajala au kavusha mlo kuna utofauti hujisikia. Utofauti huo waweza kuwa upungufu wa nguvu mwilini, kizunguzungu, na wengine hujisikia uwepesi wa mwili. Wewe ukishikwa na njaa unakuwaje au tabia gani hujitokeza? Watu wanamitindo mbalimbali ya ulaji. Mitindo ya idadi ya milo, wakati wa kula, aina ya vyakula na kiasi cha chakula na hii hutokana na sababu kadhaa. Sababu kama za kiuchumi, mazoea, ratiba ya mtu, sababu za kidini, umri, hali ya mwili na kiafya ya mtu husika pamoja na mazingira na upatikanaji wa vyakula. Kama picha inavyoonyesha hapo watu 4500 walioonyesha wao hula milo mingapi ndani ya masaa 24 yani milo kwa siku. Wapo wa mlo mmoja hadi milo minne na kuendelea. Kwani wewe unakula milo mingapi kwa siku na kwa nini? Wa...

Nafasi ya Maziwa katika Afya Zetu.

Image
MAZIWA MAZIWA MAZIWA! Tulipokuwa shuleni tulijifunza makundi ya Wanyama kulingana na sifa zao. Moja ya kundi hili ni mamalia ambao sifa yao kuu ni Wanyama wanaonyonyesha akiwemo popo, binadamu, mbwa, ng’ombe, mbuzi, kondoo nk. Wanyama hawa hufanya hivi kwa kipindi fulani na kuacha kunyonyesha mtoto/watoto wao. Kwa mfano, ndama wa ng’ombe huachishwa akiwa na umri wa miezi 4 hadi 5, baadhi ya jamii za nyani huendelea kunyonyesha watoto wao hadi wanapofikia umri wa miaka 4 wakati tembo huendelea kumnyonyesha mtoto wake hata akiwa na umri wa Zaidi ya miaka 2. Hii ina maanisha kila mnyama anaezalisha maziwa ni kwa ajili ya mtoto/watoto wake tu. Pia tutakubali kuwa kila mnyama ana tabia zake katika kumuachisha mtoto wake kunyonya. Kwa binadamu, inashauriwa mtoto anyonyeshwe hadi atakapotimiza umri wa miaka 2 na ikiwezekana aendelee kunyonyeshwa, ingawa watu wengi hawafanyi hivyo. Wengine huishia mwaka mmoja na nusu na kuacha kumnyonyesha mtoto wake. Leo ni kilele cha maadhimisho ya Siku ya m...

Afya ya Akili na uharifu katika Jamii.

Image
Siku moja tutaandaa jukwaa litakayoelezea namna afya ya akili inavyochochea uharifu katika jamii. Matukio mengi ya kiharifu yatokeayo kwenye jamii na yanayoripotiwa polisi yanachangiwa sana na matatizo ya kiakili ya wanajamii kuliko umaskini, tamaduni, sera na umiliki wa silaha. Na, Charles Msigwa.

Shairi: IWAJE?

Image
Wewe ulitakaje? Shule za msingi Vitu vifanyikaje? Katikati ya vipindi Watoto walaje? Kwa elimu-ushindi Mimi kama wewe Nina uwezo kufikiri Nafikiri mwenyewe Siwezi shikiwa akili Mwenye haki apewe Vinginevyo ni ukatili Haki ya kuelimika Na malezi stahiki Hakizo kuzishika Mtoto huwa rafiki Mzaziye wajibika Utajaona mantiki Mapumziko wasile! Darasani waingie Njaa iwazingile Somo lisiwaingie Shule waikimbie Maoniyo niambie? Wale chakula vizuri Darasa changamfu Wasipate tena sifuri Utoro ugeuke hafifu Wawe watoto wazuri Wenye afya nadhifu. Changia mawazo Tupate mwongozo Tuwajengee uwezo Elimu bora ni nguzo Hatua hizi mwanzo Tuvishinde vikwazo

Mtoto wa Afrika

Image
Siku ya Mtoto wa Afrika. Ni leo tarehe 16 mwezi Mei siku ambayo Tanzania na nchi zingine za Afrika zinaungana kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika.  Kauli mbiu ya mwaka huu ni  "Maendeleo Endelevu 2030: Imarisha Ulinzi na Fursa Sawa kwa Watoto” Kauli mbiu hii inawahimiza wazazi, walezi, jamii, Serikali na wadau wengine kuzingatia wajibu wetu katika kuimarisha mifumo ya ulinzi na maendeleo ya Mtoto ili aweze kudhibiti changamoto ya ongezeko la vitendo vya ukatili nchini pamoja na kutoa haki sawa kwa watoto wote bila ubaguzi wa aina yoyote. Awali ya yote, chimbuko la Maadhimisho haya ni Azimio lililopitishwa na uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) mwaka 1990 kwa lengo la kuwakumbuka watoto wa kitongoji cha Soweto nchini Afrika ya Kusini waliouawa tarehe 16 Juni, 1976 kutokana na ubaguzi wa rangi. Watoto hao walikuwa wakidai haki zao za kutobaguliwa pamoja na haki nyingine za kibinadamu ikiwemo haki ya kupata elimu bora na hivyo kupinga mifumo ya elimu ya kibaguzi. Kufuatia tuk...

Siku ya Maziwa Duniani. Tusherekee au Tusimame na Kujitafakari?

Image
MAZIWA MAZIWA MAZIWA! Tulipokuwa shuleni tulijifunza makundi ya Wanyama kulingana na sifa zao. Moja ya kundi hili ni mamalia ambao sifa yao kuu ni Wanyama wanaonyonyesha akiwemo popo, binadamu, mbwa, ng’ombe, mbuzi, kondoo nk. Wanyama hawa hufanya hivi kwa kipindi Fulani na kuacha kunyonyesha mtoto/watoto wao. Kwa mfano, ndama wa ng’ombe haachishwa akiwa na umri wa miezi 4 hadi 5, baadhi ya jamii za nyani huendelea kunyonyesha watoto wao hadi wanapofikia umri wa miaka 4 wakati tembo huendelea kumnyonyesha mtoto wake hata akiwa na umri wa Zaidi ya miaka 2. Hii ina maanisha kila mnyama anaezalisha maziwa ni kwa ajili ya mtoto/watoto wake tu. Pia tutakubali kuwa kila mnyama ana tabia zake katika kumuachisha mtoto wake kunyonya. Kwa binadamu, inashauriwa mtoto anyonyeshwe hadi atakapotimiza umri wa miaka 2 na ikiwezekana aendelee kunyonyeshwa, ingawa watu wengi hawafanyi hivyo. Wengine huishia mwaka mmoja na nusu na kuacha kumnyonyesha mtoto wake. Leo ni kilele cha maadh...

Mfumo wetu wa mmeng’enyo wa chakula, je umesahaulika?

Image
Mfumo wetu wa mmeng’enyo wa chakula, je umesahaulika? Ukikaa ukaangalia mambo mengi kwa makini utaona kwamba watu wengi huangaika na uzuri wa sehemu za miili yao wanazoziona. Ndio maana utakuta kuna huduma nyingi sana zinazohusu kutengeneza kucha, nywele (almaarufu kama saluni), kufanya maseji ya sehemu mbalimbali za mwili, skrabu. Ingawa huduma za afya zipo maeneo mengi lakini huduma ya uchunguzi ya mfumo wa chakula haipewi kipaumbele kama sehemu kubwa ya inayoweza kutumika kutatua matatizo mengi ya afya yanayoisibu jamii. Ni mara chache sana watu wengi wakipatwa na shida za kiafya hufikilia kuhusu afya ya mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Hii sio kibongo bongo tu bali hata nchi za wenzetu suala hili halipewi kipaumbele na watu wa kawaida pamoja na wale walioelimika katika sekta ya afya (wataalamu wa lishe, madaktari, wafamasia n.k) Hii ina maana kwamba kuna uwezekano mkubwa, matatizo mengi ya afya zetu yanaweza yakawa yanatokana na shida zilizopo katika mfumo huu kwa unafanya kazi kubw...